MWENYEKITI AVAMIWA AKATWA MKONO NA KICHWA, KICHWA CHAKE NA VIUNGO VYA SIRI VYACHEMSHWA


                                         


Mnamo 22/01/2015 majira ya 23:45hrs huko kijiji cha Songambele wilaya ya Mlele, Richard Madirisha, msukuma, 31yrs,mkulima, akiwa amelala na make wake ghafla alivamiwa na watu wasiojulikana karibia watano ambapo walivunja mlango na kuingia ndani na kuanza kumkatakata mapanga, kutenganisha kichwa, sehemu za siri kisha kuchemsha viungo hivyo nje ambapo moto ulikuwa unawaka.

Sufuria za kuchemshia viungo hivyo walivichukua ndani ambapo walimtishia mke wa marehemu aitwaye Mekrina Moses, msukuma, 25yrs asipige kelele. 

Baada ya kukamilisha zoezi walinawa mikono kwa kutumia sabuni iliyokuwa nyumbani kwa marehemu na kuondoka na simu ya marehemu yenye namba 0783846414. 

Taarifa za awali inaonyesha chanzo kulipiza kisasi kwani marehemu alikuwa akiishi Kaliua mkoani Tabora na huyo mwanamke alikuwa ni mke halali wa Shija Manyama wa kaliua hivyo marehem alipora. 

Kitendo hicho kilimuudhi Shija na kuamua kukata mapanga ng'ombe 7 wa marehemu na ugomvi ukawa unaendelea hadi July 2014 ambapo marehemu alihamia kijiji cha Songambele wilaya Mlele, na hata hivyo inasemekana vitisho viliendelea kutolewa na Shija dhidi ya marehemu kwa njia ya simu.

Jitihada za kuwatafuta watuhumiwa zinaendelea.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA