Posts

Showing posts from January, 2015

DAMU,AGANO NA SADAKA

Image
Agano ninini? Agano ni mapatano  au makubaliano kati ya mtu na mtu, mtu na Mungu au mtu na mizimu. Agano la Mtu na mizimu Agano hili hufanyika kwa njia ya damu na sadaka, Mtu anapoenda kwa mganga wa kienyeji na kuchanjwa chale tayari ameshafanya agano kwenye madhabahu ya mganga wa kienyeji ambaye ni wakala wa shetani. Hivyo anapotoa ile damu tayari umeshajiunganisha na madhabahu ile wewe ni mtumwa wa kuzimu hivyo huwezi kufanya jambo lolote bila idhini/ruhusa ya hao ‘’waliokununua‘’ kwa damu yako mwenyewe . (KUTOKA 34:12) Ujihadhari nafsi yako usije ukafanya maagano na wenyeji wa nchi ile unayoiendea usije ukawa mtego katikati yako. 13 Bali utabomoa madhabahu zao na kuvunja vunja kazi zao  na kuyakata maashera yao. 15 Usije ukafanya agano na wenyeji wan chi watu wakaenda kufanya uzunzi na miungu yao na kuitolea sadaka miungu yao mtu mmoja atakuita ukila sadaka yake. (WALAWI 17:11) Kwakuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu,name nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madha

BABA WA P SQUARE ALIFARIKI NOV.2014 AMEZIKWA JANA

Image
Mzee  Moses Okoye , baba mzazi wa mastaa wa muziki kutoka Nigeria,  Peter  na  Paul Okoye wa kundia la  ‘ P Square’  alifariki November 25 2014 baada ya kuanguka kwenye ngazi ndani ya nyumba. Taarifa za wanafamilia zilisema mzee huyo alifanyiwa upasuaji wa goti siku za nyuma na hali yake ilianza kuwa sawa kabla ya kufariki ambapo leo January 30, 2015 ndio mzee huyu amezikwa ikiwa ni miaka miwili imepita toka kufariki kwa mama yao. Hizi ni picha za safari ya mwisho ya Mzee  Moses Okoye , baba wa mastaa mzazi wa  P Square  na  Jude ‘Engees’ Okoye . Peter  na  Paul Okoye . Peter  na kaka yake  Jude Okoye . Kulikua na ulinzi pia

NEYMAR AWA TATIZO LIGI YA HISPANIA

Image
Kiungo mshambuliaji wa Barcelona Neymar Da Silva Jr vamekuwa kwenye kiwango cha juu msimu huu ambapo amekuwa sehemu muhimu sana ya timu yake katika michezo ya hivi karibuni . Neymar amedhihirisha ubora wake kwa jinsi ambavyo amekuwa akifunga mabao mfululizo huku akisaidia kwa kutoa pasi za mwisho kwa wenzie na amekuwa akifanya hivyo kwa mwendelezo mzuri , Tatizo limekuwa moja tu , jinsi amabvyo mchezaji huyu amekuwa akilaumiwa hasa na wapinzani kwa kuwa mtovu wa nidhamu na mkosefu wa heshima ambapo amekuwa akiwadhihaki wachezaji wa timu pinzani kwenye nyakati tofauti hali ambayo imeonekana kuwakera wengi . Wapinzani wa Barcelona wamemlalamikia Neymar kwa kitendo chake cha kuwadhihaki anapokuwa uwanjani . Neymar amekuwa na tabia ya kuwatukana wachezaji wa timu pinzani na wakati mwingine hata kwa vitendo na ndio maana amekuwa kwenye vurugu nyingi ambazo zimekuwa zikitokea kwenye michezo ya Fc Barcelona . Majuzi wakati wa mchezo war obo fainali ya michuano ya Kombe

CHENGE AGEUKA MBOGO BUNGENI KWA KUITWA FISADI,

Image
Amtaka Halima Mdee athibitishe Mbunge Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) ametakiwa kuwasilisha ushahidi kuthibitisha kauli yake ya kumtuhumu Mbunge Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), kwa ufisadi.   Chenge alilazimika kuomba utaratibu wa kiti juzi, baada ya Mbunge huyo wa Kawe kumtaja mara mbili wakati akichangia mjadala wa taarifa za kudumu za Bunge zilizowasilishwa juzi.   Mara ya kwanza, Mdee alimhusisha Chenge na mkataba mbovu wa Kampuni ya Ndege (ATCL) uliosababisha Serikali kuingia hasara ya zaidi ya Sh bilioni 90.   Licha ya kumtaja kwenye ufisadi huo ambao kwa mujibu wa Mdee, Chenge ndiye alikuwa Waziri wa Wizara yenye dhamana na ATCL, pia alimtaja kuhusika katika kashfa nyinginezo ikiwemo suala la utoaji takribani Sh bilioni 200, katika iliyokuwa Akaunti ya Tegeta Escrow ya Benki Kuu (BoT).   “Wabunge tuanze kuchunguzana humu ndani na kushughulikiana,” alisema Mdee na kutaja kwamba kwa kuanza, waanze na Che

BABA AJIUA KWA KUONA PICHA ZA UTUPU ZA BINTI YAKE

Image
Wazazi wamekua na nafasi kubwa sana katika malezi ya watoto wao hata wakati pale wanapokuwa watu wazima lakini baba huyu kutokana na upendo kwa mwanaye aliamua kujiua baada ya kuona picha za mtoto wake alizopiga akiwa mtupu katika jarida la Playboy   nchini  Romania. Loredana Chivu  anayeishi aliamua kuweka picha hizo akiwa amepiga katika staili tofauti katika mitandao mbalimbali ya kijamii ambapo baba yake baada ya kuziona alimkana mwanaye huyo. Loredana Chivu   msichana aliyesababisha kifo cha baba yake Kwa mujibu wa mtandao wa  The Mirror , msichana huyo akisimulia kwa machungu baada ya kifo cha baba yake alisema hakutegemea kama ipo siku baba yake angekasirika kiasi cha kujitoa uhai.

AMCHINJA MKE WAKE GESTI NA KUMTOA MOYO NA MAINI

Image
Huu ni ukatili namba moja kwa wanandoa duniani! Bado picha haijatoka kichwani kwa wakazi wa Manzese jijini Dar kufuatia kifo cha kuchinjwa cha  Josephine Ndengaleo Mushi kinachodaiwa kufanywa na mume wake wa ndoa, Remy Joseph (35). Tukio hilo la kutisha kusimuliwa achilia mbali kuona, lilijiri saa 9: 10 alasiri ya Januari 29, mwaka huu ndani ya chumba kimoja kilichopo ghorofa ya pili ya  Hotel Friend’s Corner Ltd iliyopo Manzese Argentina, Dar. Baada ya habari za mauji hayo kusambaa kama moto wa kifuu, waandishi wetu walianza kuichimba habari hii kwa kina. Kwa mujibu wa mhudumu mmoja wa hoteli hiyo, Januari 28, mwaka huu, Remy na Josephine walifika kwenye hoteli hiyo na kuchukua chumba. Walionekana wenye amani, kwani hakuna sura iliyoonesha kuna tatizo. “Walikuwa kama wateja wengine. Tena niliwauliza kama wanatoka mkoa, wakasema ni wakazi wa Dar es Salaam, wao ni mke na mume kwa ndoa, waliamua kulala hapa ili kuimarisha mapenzi yao, si lazima kila siku nyum

MAGAZETI YA LEO JAN 30/2015

Image
. . . . .

DENTI WA CHUO KIKUU MWAKA WA MWISHO ALA KICHAPO KWA KUIBA BASKELI

Image
Amebakisha miezi mnne tu kumaliza chuo denti wa chuo kikuu cha Jordan, Morogoro anayeitwa Somi Endless mekamatwa akiiba baiskeli iliyokua imeegeshwa  maeneo ya chuoni hapo. kijana huyo anayefahamika kwa jina la Somi Endless ambaye anasomea ualimu akiwa  mwaka wa tatu yaani amebakiza miezi kama 5 hv amalize chuo inasemekana ni mtumiaji  mzuri wa bangi na hata mahudhurio yake darasani ni ya shda Aliokolewa na polisi na kupelekwa kituoni kwa mahojiano zaidi.

SISTER WA KANISA KATOLIKI AJIFUNGUA MTOTO

Image
Utata umeibuka  baada ya sister wa Kanisa Katoliki huko  Italy  aliyekuwa akilalamikia maumivu ya tumbo na kukimbizwa Hospitali na kujifungua mtoto wa kiume licha ya kuishi katika Jumuiya hiyo ya wanawake watupu.    Sister huyo  mwenye umri wa miaka 31 yupo kwenye kikundi cha masista cha  Santa Chiara  Italy, asili yake ni Amerika ya Kusini, alilalamikia maumivu makali  ya tumbo baadaye alianguka, madaktari walifika katika eneo hilo na baada ya kumfikisha Labour alijifungua.   Watu wengi wameshindwa kuelewa kwa jinsi gani ameweza kupata ujauzito licha ya kula kiapo cha usafi wa moyo na utii.   Tukio linalofanana na hili lilitokea mwaka jana baada ya sister mmoja wa Salvador ambaye umri wake ni miaka 33 ambaye alijifungua mtoto wa kiume na kumpa jina la Papa Francis.

BUNGE LAJADILI KIPIGO CHA LIPUMBA MJADALA WOTE HUU HAPA

Image
Leo Bunge Limejadili  hoja ya dharura ya Mh.Mbatia juu ya kupigwa kwa Mh.Lipumba wakati wa mkutano wake na wananchi wakati wa kumbukumbu ya mauaji ya wenzao waliokuwa wamefariki Pemba 2001.   Hoja hiyo imejadiliwa kwa mujibu wa kifungu cha 47  ambapo  msemaji  wa  kwanza  alikuwa  ni  Waziri  wa  Mambo  ya  ndani  ya  nchi ambaye  alisimama  kutoa  msimamo  wa  serikali.   Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Chikawe: Kufatia hoja ya Mh James Mbatia Mbunge ninamaelezo yafatayo, Tar 26 Jan Jeshi la polisi lilipokea barua kutoka Chama cha CUF. Barua hiyo ilikuwa ikitoa taarifa za kufanyika kwa maandamano kwenye viwanja vya Zackiem MBagara.   Maandamano yalipangwa kuanzia Temeke kuelekea Zackiem, Jeshi la polisi liliwaita viongozi wa CUF kwa mazungumzo. Walifanya mazungumzo na jeshi la polisi lilitoa tahadhari kadhaa kutokana na sababu za kiusalama. Viongozi wa CUF waliridhika na ushauri wa kamanda SIRO. Katika hali ya kushangaza Profesa Ibrahimu Lipumba alikaidi Zuio la Jeshi l