Posts

Showing posts from January, 2018

Sababu za Roberto Carlos kuamini CR7 ni bora kuliko Messi

Image
Mjadala mkubwa katika soka ulimwenguni kwa sasa ni juu ya uwezo wa wachezaji wawili mmoja anakipiga Real Madrid na mwingine yuko Barcelona pale, ndio ni Cristiano Ronaldo na Lioneil Messi. Mjadala wa Messi na Ronaldo unaonekana mpana sana na kila mtu ana sababu zake kumkubali huyu na kumkataa huyu, na hata kwa beki wa zamani wa Brazil Roberto Carlos naye ana sababu za kumkubali zaidi CR7. Carlos anaamini kwamba Cristiano Ronaldo ni bora zaidi ya Lioneil Messi kwani amekuwa akimuona Ronaldo mazoezini jinsi amekuwa akijituma na pia juhudi zake mazoezini anavyozionesha uwanjani. Carlos anasema tofauti kati ya Messi na Ronaldo ni kwamba Ronaldo anajituma sana akiwa uwanjani na pia mazoezini kiyu ambacho Lioneil anaonekana kukikosa na zaidi anaamini katika kipaji chake. Carlos amewahi kuichezea Real Madrid kwa miaka zaidi ya 14 kabla yakuondoka kutoka kwa wababe hao wa Hispania mwaka 2007 ambapo alikwenda kujiunga na klabu ya Fernabache ya nchini Uturuki.

HABARI ZILIZOPO KWENYE MAGAZETI YA LEO JAN 5. 2018

Image
Friday, January 5, 2018