MWANANKE HUYU AFUNGA NDOA NA PAKA


2472B70300000578-0-image-a-5_1420544912306
Dunia haishi maajabu na maajabu yamekuwa yakitokea siku hadi siku na yanatokea karibu kila mahali.
Mwanamke mmoja huko nchini Marekani aitwaye Barbarella Buchner ametoa kali ya mwaka 2015 baada ya kufunga ndoa na paka wake wawili.
Mwanamke huyo alipokuwa anatoa ufafanuzi juu ya tukio hilo amesema kuwa hakuwahi kuwa na wazo la kuolewa na mpenzi yoyote yule wa kiume kati ya wapenzi alio nao na hajawahi kuwa na wazo kwamba atakuja kuwa mke wa mtu au kiumbe yoyote yule.
Barbarella Buchner akiwa na paka wake wawii aliofunga nao ndoa hivi karibuni.
Barbarella Buchner akiwa na paka wake wawii aliofunga nao ndoa hivi karibuni.
Barbarella mwenye umri wa miaka 48 ambaye kazi yake ni ubunifu wa tovuti kwenye mtandao wa internet ameongeza kuwa ana furaha kubwa baada ya kuolewa na paka wake wawili ambao ameolewa nao.
Mwanamke huyo alinukuliwa akisema kuwa “Kuna baadhi ya wanawake wamepangiwa kufanya usafi kwa ajili ya waume zao na wameridhia kufanya hivyo , kwangu ni tofauti“– Barbarella.
Barbarella Buchner akiwa na mmoja kati ya waume wake ambao ni paka.
Barbarella Buchner akiwa na mmoja kati ya waume wake ambao ni paka.
Ameongeza kuwa haoni shida kuwatumikia paka wake ambao wana majina ya Lugosi naSpider na siku zote atahakikisha wanaishi kwa furaha kama ndoa inavyohitaji.
Mwanamke huyu hakuweza kufananua kama moja ya misingi muhimu ya ndoa ‘unyumba’ itahusika kwenye ndoa yake hiyo na paka wake wawili.
2472B48800000578-0-image-m-21_1420545104078
Cheti cha ndoa ya Barbarella Buchner na pake wake Spider na Lugosi kinachodhirisha uhalali wa ndoa yao.
Cheti cha ndoa ya Barbarella Buchner na pake wakeSpider na Lugosi kinachodhirisha uhalali wa ndoa yao.
2472B94B00000578-0-image-a-7_1420544933525

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA