Posts

Showing posts from April, 2015

GODBLESS LEMA AMSHAMBULIA ZITTO KABWE, AMTUHUMU KUIKOSESHA USHINDI CHADEMA

Image
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewatoa hofu wanachama wake mkoani Shinyanga kikidai propaganda zinazoenezwa na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Bw. Zitto Kabwe, anayedai chama hicho kimepoteza mwelekeo si za kweli bali ni uongo. Mbunge wa Arusha Mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Taifa, Bw. Godbless Lema, aliyasema hayo hivi karibuni mkoani Shinyanga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mahakama ya Mwanzo. Alisema chama chao bado kipo imara na hakitagawanyika kama inavyodaiwa na Bw. Kabwe ambaye CHADEMA kilimfukuza katika chama baada ya kukisaliti hivyo kukiuka Katiba ya chama hicho. "Ndugu zangu wana Shinyanga, CHADEMA tupo imara na tutaendelea kuwa imara hadi tukamate dola na kuwakomboa Watanzania ambao wanateseka tangu tupate uhuru. "Zitto hana ubavu wa kukigawa chama chetu kama anavyofikiri na kuamini...anahangaika bure, alitaka kukiua tukamshtukia na mimi ndiye mtu wa kwanza kubaini njam

RAFIKI WA NGUVU TUMA TFA 130 KWENDA 15522,SAMBAZA UPENDO KWA KUMPIGIA KURA MRISHO ZIMBWE

Image
"Marafiki ndugu zangu na mashabiki zangu wa  ukweli support   yenu kwangu niweze kupata tuzo T F A 130  kwenda 15522 asante kwa kunipigia kura na kuibuka na tuzo  ONE LOVE"

BAADA YA KUMFUMANIA MKEWE NA SERENGETI BOY WA MIAKA 16, MUME ADAI MKE WAKE ANAMAPEPO

Image
Tumaini Mwashambo anayedaiwa kupigwa na mumewe. SHANGAA! Mwanamke mmoja aliyetajwa kwa jina la Tumaini Mwashambo (28), mkazi wa Mtaa wa Half Londan, Kata ya Sogea wilayani Momba, Mbeya amejikuta akipokea kipigo kikali kutoka kwa mumewe, Jamsoni Vicent (34) akidai amemfumania na mtoto wa miaka 16 ‘Serengeti boi’. Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Jamsoni alisema ni mara ya pili kumfumania mke wake na huyo mtoto ambapo alisema anaamini ni sawa na kumbaka. “Mara ya kwanza niliwakuta wanaangalia mkanda wa ngono huku wakiwa peke yao, yeye na mtoto huyo kwenye nyumba yangu. Nilimuonya Tumaini kuwa tabia hiyo si nzuri lakini hakutaka kunisikiliza,” alidai mwanaume huyo. Aliendelea kudai kuwa, mara ya pili alimkuta tena mkewe huyo akiwa amempakata mtoto huyo huku wakilishana mayai, pia mke akiwa amevaa kanga moja. “Nilishangaa sana mke wangu kuwa na tabia kama hiyo ya ubakaji lakini niliishia kumuonya tu. Kweli za mwizi ni arobaini kwani nilikuja kumkamata mke wangu ak

MSHTUKO: WACHINA WANASWA WAKITENGENEZA CONDOMS FEKI MILIONI 3

Image
Three million fake condoms confiscated in Shanghai Shanghai police busted an illegal  ‪#‎ condom‬ workshop on Tuesday, and confiscated about 3 million fake condom s. The fake goods were all produced inside the well-equipped workshop, and were sold online under big name brands such as Durex and Jissbon to small hotels. While the online cost was only 0.1 yuan ($0.016) per item, the hotels made a hefty profit by selling them to customers for around 3 yuan ($0.5), according to Xin’an Evening News.Zhang Wenliang, a Shanghai police officer on the case, explained that the issue was more than just about using fake branding. “The materials used in these products are of very low quality, and have a disgusting smell,” said Zhang, “Heavy metal elements were tested in them, which are very harmful to the human body.” The case involved over 12 million yuan ($1.9 million) at large. Up to eight municipalities and provinces in China, including Shanghai, Guangdong and Shaanxi, have seen the

ILI KUWALINDA WASIOWEZA KUSEMA HAPANA,WENYE HIV KUWEKWA ALAMA ILI KUWATAMBUA

Image
Radiocity 97FM LAW PASSED: ALL HIV POSITIVE PEOPLE WOULD BE MARKED NEAR THEIR GENITALS President Zuma signed a bill that seem to be the greatest step in history of trying to c ombat HIV. From now on every person who gets tested and found to be HIV positive would not just get  counselling and medication. They would also get a mark in a form of a tattoo near their genital according to the bill singed by the president. “The mark is to protect those who can’t say no to sex. I mean if you can’t read between the lines you should read between the legs because that’s where the status would be tatted. The choice to be HIV positive is now in your hands or your genitals for that matter….We also encourage those who had been living with the virus to go to the nearest public hospitals to get their status tatted in”. Said Jacob Zuma after signing the bill and drinking his ARV’s. WILL MARKING ALL HIV POSITIVE PEOPLE REDUCE ITS PREVALENCE RATE?

HONGERA BOSS WA TANURU LA FIKRA KUVUTA JIKO

Image
Blog ya nyumbani inachukua fursa hii kumpongeza sana mtu wa watu Sambala Ole Comrade Mmiliki wa kundi maarufu katika mtandao wa Facebook lijulikanalo kama TANURU LA FIKRA lenye watu zidi ya 90,000 linalosaidia watu wengi tunasema tena hongera sana kwa kuamua kuachana na ukapera na kuvuta jiko, 

SAKATA LA ASKOFU KUZAA NJE YA NDOA LACHUKUA SURA MPYA

Image
Askofu Benson Bagonza LILE  sakata la Peace Sylvester (36), mkazi wa Kijenge jijini hapa kudai amezaa watoto wawili na Askofu Benson Bagonza wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Karagwe mkoani Kagera limechukua sura mpya baada ya Peace kuibua mambo mapya. Akizungumza na gazeti hili Jumamosi iliyopita, Peace alisema kuwa, amefuatwa na mtu aliyedai ametumwa na askofu huyo kumpa shilingi 400,000 kama nauli ya kwenda kwao Karagwe kwa ajili ya suluhu na askofu huyo. Pia Peace alibainisha kwamba, baadhi ya viongozi wa kanisa hilo wanafanya mipango ya chini kwa chini kwa kuwatumia baadhi ya waandishi wa habari ili kukutana naye kwa lengo la kumshawishi akanushe taarifa iliyotoka kwenye gazeti hili Jumatatu iliyopita. “Kuna mwandishi wa habari anaitwa…(anamtaja jina) amekuja hapa Arusha akitokea Dar kwa ajili yangu. Huyu mwandishi amekuwa akinipigia simu mara kwa mara akitaka tukutane ili anishawishi nikanushe zile habari nilizotoa kwamba nimezaa na askofu

AKIMBIWA NA MKE BAADA YA MGUU WAKE KUOZA

Image
“NAJUTA kuzaliwa, sikujua kama maisha yangu yangebadilika kuwa katika hali hii! Mke amenikimbia, jamii imenitenga, sina rafiki, ndugu nao hawanipendi. Haya yote yananikuta kwa sababu ya huu ugonjwa ambao sikuuomba,” ndivyo alivyoanza kusema huku akilia, Seleman Juma (pichani). Seleman mwenye miaka 38 na mkazi wa Vingunguti jijini Dar amekimbiwa na familia yake kutokana na ugonjwa wa Matende unaomsumbua na amejikuta akiishi peke yake katika mazingira yasiyostahili binadamu kuishi.  HISTORIA FUPI YA MAISHA YAKE  “Mimi ni mtoto wa tatu kati ya wanne, katika familia yetu. Tulizaliwa Kijiji cha Masimba wilayani Kisarawe, Pwani, nimebaki na mama baada ya baba kufariki dunia mwaka 2010. “Sina elimu yoyote, kwani sijawahi kwenda shule hata chekechea, naamini wazazi wangu walichangia.  “Mwaka 1997, kutokana na ugumu wa maisha niliamua kuja jijini Dar kutafuta, nikawa nafanya kibarua katika Machinjio ya Vingunguti “Mwaka 1999 nilimuoa Aisha Salum. Mwaka 2002 a

MVUA YAUWA WAWILI TANGA

Image
Watoto wawili wamekufa huku wengine wawili wakijeruhiwa vibaya baada ya ukuta wa nyumba waliyokuwa wamelala kuwaangukia na kuwafunika kitandani kufuatia mvua kubwa inayoendelea kunyesha mkoani Tanga. Wakizungumza na Mpekuzi katika eneo la tukio lililopo barabara ya 18 jijijni Tanga viongozi wa serikali na wale wa wananchi wa eneo hilo wamesema limetokea juzi majira ya saa 11 Alfajiri wakati mvua iliyoambatana na upepo ikinyesha ndipo ukuta wa nyumba hiyo uliojengwa na mawe makubwa ya baharini ulipodondoka na kusababisha madhara hayo.   Waliokufa katika eneo hilo wametajwa kuwa ni Bakari Shabani mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Ngamiani kati na Hassan Abdala mwenye umri wa mwaka mmoja ambao walifariki papo hapo huku wengine wawili wakijeruhiwa vibaya akiwemo mama mzazi wa marehemu ambao wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo.   Kufuatia hatua hiyo diwani Mbaruk ameiomba halmashauri ya jijij la Tanga pamoja na idara ya majengo kufanya uk

VURUGU BURUNDI POLISI WAPAMBANA NA WAANDAMAJI WANAOMPINGA NKURUNZINZA, NCHI HIYO HAIRUHUSU URAIS MIHULA MITATU

Image
WAPINZANI wa Serikali nchini Burundi, wameitisha maandamano makubwa leo ya kupinga hatua ya Chama Tawala cha CNDD-FDD kumtangaza Rais Pierre Nkurunziza, wa nchi hiyo kuwania mhula wa tatu katika uchaguzi ujao (Katiba ya Nchi hiyo hairuhusu mihula mitatu). Mkuu wa Chama cha FNL kilichipigwa marufuku nchini humo, Agathon Rwasa, amepinga vikali uamuzi huo na kusema kwamba unaenda kinyume na Katiba ya Burundi. Rwasa, amesisitiza kuwa, kuteuliwa kwa Rais Nkurunzinza kw aajili yam hula wa tatu utaitumbukiza nchi hiyo katika matatizo makubwa. Rwasa ndiye aliyekuwa mpinzani mkuu wa rais Pierre Nkurunziza katika uchaguzi mkuu wa mwezi Juni, 2010. Kufuatia hatua hiyo, wapinzani hao wa serikali kwa nyakati tofauti, wameitisha maandamano makubwa leo Aprili 26, 2015 kupinga hatua hiyo ya chama tawala. Akimtangaza rasmi Rais Nkurunzinza, Mwenyekiti wa Chama Tawala nchini humo, Pascal Nyebenda, aliwataka wapinzani wa serikali kuwa watulivu na kuachana na Rais Nkurunzinza katika m

ACT-WAZALENDO WABADILI JINA

Image
Chama kipya cha ACT-Wazalendo kinachoongozwa na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (pichani juu), kimebadili jina lake la awali la ACT-Tanzania. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini imekubali maombi ya chama hicho huku ikiwataka kurudisha cheti cha usajili wa awali na kupewa cheti kingine. Awali ACTL-Wazalendo ilipata usajili kwa jina la ACT-Tanzania na baadae kuomba kulibadili jina hilo. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, ameridhika na maelezo yaliyokuwa yametolewa na uongozi wa chama hicho wa sababu za kuamua kubadili jina la chama hicho kutoka ACT-Tanzania hadi ACT-Wazalendo. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwa vyombo vya habari jana jiijini Dar es Salaam, Jaji Mutungu alijibu ombi hilo kwa njia ya barua. Katika taarifa hiyo inaeleza: "Nikurejeshe kwenye barua yenye kumbukumbua namba AC-HQ/MSJ/2015 ya Aprili 15, mwaka 2015 ikisomwa sambamba na barua yangu yenye