KIGOGO BENKI KUU KIZIMBANI KWA JARIBIO LA KUTAKA KUUA POLISI



Mshauri wa masuala ya ulinzi katika Benki Kuu (BoT), Shaban Ndosi (39) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya kujaribu kumuua ofisa wa Polisi.

Ndosi alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande Lema. 
 
Wakili wa Serikali, Janeth Kitali alidai kuwa Oktoba 21, 2014 katika eneo daraja la Salender karibu na mataa ya kuongoza magari, alijaribu kumuua askari Polisi, Koplo Salehe.
 
Hakimu Lema alisema mshitakiwa hatakiwa kujibu mashitaka kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na upelelezi umeshakamilika hivyo kesi itahamishiwa Mahakama  Kuu.
 

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA

MAGONJWA 27 YANAYOTIBIWA NA ASALI YENYE MDALASINI