MWANAFUNZI AJIFUNGUA NDANI YA DALADALA



Mwanafunzi mmoja wa Shule ya Sekondari ya Keko amejifungua mtoto akiwa ndani ya daladala maeneo ya Mtoni Kwa Azizi Ally, jijini Dar es Salaam juzi  tarehe 23.
 
Mwanafunzi huyo ambaye hakuweza kupatikana jina lake mara moja, anasemekana alijifungua mtoto huyo bila ridhaa yake wakati akiwa katika harakati za kuitoa mimba hiyo.
 
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, msichana huyo anasemekana alikuwa amekunywa madawa makali kwa lengo la kuitoa mimba hiyo ambayo anadaiwa kuificha  hadi pale alipoumbuka mchana wa siku hiyo.
 
Haikuweza kufahamika mara moja alikopelekwa mtoto huyo baada ya tukio hilo wala hatua alizochukuliwa binti huyo.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA