MSANII WA TMK WANAUME FAMILY ''YP'' AZIKWA LEO MAKABURI YA CHANG'OMBE JIJINI DAR


Wasanii wa Bongo Fleva wakiuaga mwili wa marehemu Yesaya Ambikile 'YP' katika Viwanja vya TCC Chang'ombe, Dar es Salaam.
Waombolezaji wakiwa katika msiba wa msanii wa Bongo Fleva, Yesaya Ambikile 'YP' kwenye Viwanj vya TCC, Chang'ombe, Dar.


Mke wa marehemu YP, Sakina Robert (mwenye kiremba cheupe) akiwa katika hali ya majonzi.
Msanii wa Bongo Fleva, Juma Nature akizungumza jambo kwa niaba ya wasanii wenzake waliofanya kazi na marehemu enzi za uhai wake.
Baadhi ya wasanii na waombolezaji wakiwa mbele ya jeneza muda mfupi kabla ya kuuaga mwili wa marehemu.



Juma Nature akifunua jeneza tayari kwa shughuli ya kuuaga mwili huo.
Mtoto wa marehemu, Ambikile Yesaya akisogezwa mbele ye jeneza kuuaga mwili wa baba yake.

Msanii wa filamu, William Mtitu akipita kuaga mwili wa marehemu
Msanii wa vichekesho, Mussa Kitale 'Mkude Simba' akiaga mwili.

Sehemu ya mamia ya waombolezaji wakiwa makaburini.
Maombolezaji wakiwa wamebeba jeneza kwenda makaburini.

Waombolezaji wakiwa wamebeba bango lenye picha ya marehemu.
Jeneza likishushwa kaburini.

MSANII WA TMK WANAUME FAMILY, Yesaya Ambikile 'YP' aliyefariki usiku wa kuamkia janai, amezikwa leo katika makaburi ya Chang’ombe maduka mawili jijini Dar jioni hii. Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie waliokuwepo kuungana na wasanii wenzao wa Bongo Fleva ni pamoja na JB, Steve Nyerere, Jacqueline Wolper, Kajala Masanja, Shilole, William Mtitu, Mkude Simba na wengineo.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA