LULU: SINA LA KUSEMA JUU YA KIFP CHA SEKI

INASIKITISHA SANA: Mwanadada LULU afiwa na mpenzi wake LEO siku ya birthday yake

Kufuatia kuhusishwa na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na marehemu Bilionea Lusekelo Samson Mwandenga ‘Seki’ aliyefariki dunia Alhamisi iliyopita, Staa wa Bongo Movies Elizaberth Michael ‘Lulu’ amesema hana la kusema na hana tamko lolote fufuatia kifo cha Seki.

Akiongea na gazeti la Ijumaa Wikienda Juzi, lililotaka kujua taarifa za yeye kuhusishwa na bilionea huyo pamoja na mambo mengine, Lulu alijibu kwa kifupi;

Mwandishi: “Lulu kwanza tumesikia unaumwa na umelazwa, ni kweli?”

Lulu: “Siyo kweli, mimi mbona nipo tu hapa nyumbani.”

Mwandishi: “Kuna manenomaneno kuhusu kifo cha Seki, watu wanakusema vibaya mitandaoni. Je, unatoa tamko gani?”

Lulu: “Sina tamko lolote.”

Mwandishi: “Lakini ni mtu uliyekuwa unamfahamu au alikuwa mpenzi wako?”

Lulu: “Sina cha kusema mimi na sina tamko lolote.”

Alipobanwa kwa maswali zaidi kuhusiana kuwa na uhusiano na bilionea huyo, kutofanyika kwa bethidei yake na kufuta akaunti ya Instagram, Lulu hakuwa tayari kujibu lolote.

Marehemu Seki ambaye alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa madini, Arusha na Dar ameacha mke na watoto wawili.


Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA