MASTAA WANUSURIKA KIFO



Mastaa kutoka tasnia ya uigizaji Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’, Lucas Mhuvile ‘Joti’, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’, Isaya Mwakilasa ‘Wakuvwanga’, Alex Chalamila ‘Mac Regan’, Sekioni David ‘Seki’ na abiria kibao wamenusurika kufa katika ajali ya ndege.


                               Abiria wakiingia ndani ya ndege.


Kwa mujibu wa shuhuda wetu ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, tukio hilo lilijiri asubuhi ya Alhamisi iliyopita uwanjani ambapo ndege waliyopanda ya Shirika la Ndege la Fastjet aina ya FN 141 Airbus ilipata hitilafu kwenye injini ya kushoto ilipokuwa ikiruka.
                Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’.

Akizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili muda mfupi baada ya tukio hilo baya, Dude alisimulia mkasa huo kwamba, ndege hiyo ilikuwa kwenye spidi ikipaa angani ndipo ikafeli na kuanguka.
Dude alisema taarifa zilizopatikana baadaye zilidai kwamba kabla ya kuruka, ndege aina ya kunguru aliingia kwenye injini ya kushoto na ndiye aliyesababisha hitilafu hiyo kisha ndege ikakosa mwelekeo na kuserereka chini.
Alisema wakati inaserereka ilikwenda kutua kwenye majani ambapo waliokolewa na fire (zimamoto).
Baada ya abiria hao kuokolewa, waliwekwa kwenye chumba maalum kutokana na baadhi yao kutaharuki na kupandwa na presha.
                                   Kulwa Kikumba ‘Dude’.

“Tunamshukuru Mungu tumepona maana ajali ilikuwa mbaya sana.
“Tulikuwa tunaenda Mwanza kisha mimi nitaenda Bukoba na akina Masanja wataelekea Mara kwa shughuli za kisanaa.
“Hapa mimi niko sawa ila wenzangu hawajiwezi kwa presha,” alisema Dude.
Habari zilizopatikana baadaye zilisema kuwa wasanii hao na abiria wengine walipatiwa ndege nyingine wakaendelea na safari.
Juhudi za kumpata msemaji wa Fastjet, Lucy Mbogoro ili azungumzie ajali hiyo hazikuzaa matunda baada ya simu zote, ya ofisini na kiganjani kuita bila kupokelewa.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA

MAGONJWA 27 YANAYOTIBIWA NA ASALI YENYE MDALASINI