Posts

Showing posts from 2025

MWANAUME ALIYEOA WAKE 27 SIKU MOJA AISHANGAZA DUNIA

Image
Fela Kuti: Mwanamuziki Mshujaa Aliyeoa Wake 27 kwa Siku Moja na Kuandika Historia ya Afrika Katika historia ya muziki wa Afrika, jina la Fela Anikulapo Kuti linang’aa kama mwanga wa matumaini na mapambano. Alikuwa siyo tu mwanamuziki mashuhuri kutoka Nigeria, bali pia mwanaharakati shujaa, aliyeitumia sanaa yake kupinga mfumo wa kisiasa, ukoloni mamboleo, na ukandamizaji wa haki za wananchi barani Afrika. Lakini mbali na ujasiri wake kisiasa, Fela pia aligonga vichwa vya habari duniani kote mwaka 1978, kwa tukio ambalo hadi leo linaendelea kuwashangaza wengi. Katika mwaka huo, Fela aliushangaza ulimwengu kwa kuoa wake 27 kwa siku moja – jambo ambalo halijawahi kufanywa na msanii yeyote wa Kiafrika wa wakati wake. Hafla hiyo ya kipekee haikufanyika kwa siri, bali ilihudhuriwa na viongozi wa kimila 12, ambao walialikwa rasmi kufungisha ndoa hizo kwa mujibu wa mila na desturi za Yoruba – kabila kubwa alilotoka Fela. Kilichofanya tukio hilo kuwa la kipekee zaidi ni kwamba wanawake wote 27 ...

KIMBUNGA DIKELEDI KUIKARIBIA TANZANIA, WAKAZI WA MAENEO HAYA WAPEWA TAHADHALI

Image
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa rasmi kuhusu kimbunga Dikeledi kinachopitia Bahari ya Hindi karibu na pwani ya Msumbiji. Kwa mujibu wa tathmini ya hali ya hewa iliyofanywa, kimbunga hicho hakina athari za moja kwa moja kwa upande wa Tanzania, lakini kinaweza kuleta vipindi vya mvua kubwa katika mikoa ya Lindi na Mtwara. TMA imeeleza kuwa kimbunga Dikeledi, ambacho kwa sasa kipo mwambao wa Msumbiji, kinatarajiwa kurejea katika Rasi ya Msumbiji leo alasiri. Ingawa hakitathiri moja kwa moja maeneo ya Tanzania, ukaribu wake na pwani ya kusini unatoa uwezekano mdogo wa kuibuka kwa mvua kubwa na upepo mkali. Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, vipindi vya upepo mkali na mawimbi makubwa ya bahari vinatarajiwa kuathiri ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi kati ya Januari 14 na 15, 2025. Hali hii inaweza kuwa changamoto kwa shughuli za uvuvi na usafirishaji wa majini, hivyo basi watumiaji wa bahari wanapaswa kuchukua tahadhari kubwa kwa kipindi hiki. TMA ilianza kutoa tahadhari...

TAHADHALI: MVUA KUBWA KUNYESHA MIKOA HII

Image
Mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa nchini Tanzania TMA imetoa taarifa kuhusu utabiri wa hali ya hewa nchini Tanzania. Kulingana na taarifa tulizozipata hivi sasa, hali ya mawingu kiasi, mvua nyingi na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache ya mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Dar es Salaam, Mara, Morogoro na Manyara. Pia maeneo ya Kilimanjaro, Tabora, Kigoma, Katavyi, Lindi, Mtwara na Pwani yatapokea mvua nyingi na ngurumo za radi. TMA imetoa angalizo la mvua kubwa katika maeneo machache nchini Tanzania. Kulingana na taarifa tulizozipata hivi sasa, vipindi vifupi vya mvua kubwa vinatarajiwa katika maeneo machache ya mikoa ya Mtwara,Lindi, Ruvuma na Kusini mwa mkoa wa Morogoro. Maeneo Yafuatayo Magharibi mwa nchi mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora vipindi vifupi vya mvua zitakazoambatana na ngurumo za radi katika maeneo machache kwanzia leo jioni vinatarajiwa. Pia Kanda ya kati Mikoa ya Dodoma na Singida vipindi vifupi vya mvua nyepesi katika maeneo machache vinatar...

NAFASI ZA KAZI YA UHUDUMU WA NDEGE KUTOKA JOB JUNCTION TANZANIA

Image
EMPLOYER:Job Junction Tanzania LOCATION:Dar Es Salaam Minimum Education level: Bachelor JOB DESCRIPTIONS: * Provide information, guidance, and assistance for safety and comfort to passengers on board aircraft * Attend the “brief” and act on it * Conduct safety check before flight * Greet customers, check their tickets and accompany them to their seats * Prepare and serve drinks and food to passengers * Present emergency equipment and give instructions * Monitor and secure the cabin regularly * Comply with all aviation rules and regulations for safety and protection * Assist passengers and cabin crew during emergency situations * Provide special help to passengers with special needs (children, disabled persons, elders etc) * Submit analytic reports concerning flight incidents Requirements * Fluency in English, multilingual is preferred * MS Office knowledge * Customer service-oriented * Professional image * Excellent communication and presentation skills * Problem solving skills and abi...

YANGA SC YATANGAZA KUACHANA NA KOCHA MILOUD HAMDI, SABABU HIZI HAPA

Image
Klabu ya Young Africans Sports Club (Yanga SC) imepiga hatua kubwa katika mabadiliko ya benchi la ufundi baada ya kutangaza rasmi kuachana na kocha wao, Miloud Hamdi. Hamdi, raia wa Algeria na Ufaransa, aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu hiyo mnamo mwezi Februari 2025, akichukua nafasi ya Sead Ramovic aliyeondoka baada ya mkataba wao kuvunjika kwa makubaliano ya pande mbili. Mabadiliko haya yanakuja katika kipindi cha mabadiliko makubwa ndani ya klabu hiyo, huku mashabiki wakiendelea kutafuta matumaini ya mafanikio zaidi. Miloud Hamdi alikuja kwa Yanga akiwa na uzoefu mkubwa kutoka kwa vilabu mbalimbali vya soka, akiwahi kuwa kocha katika mataifa kama Algeria, Ufaransa, na maeneo mengine barani Afrika. Katika safari yake ya ukocha, Hamdi alionyesha uwezo wake kwa kushinda taji la Ligi Kuu ya Algeria na kufika hatua ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika akiwa na USM Alger. Hii ilikuwa ni ishara ya uwezo wake wa kuongoza timu katika ushindani mkali. Hata hivyo, uongozi wa Yanga ulilazimi...

UKIONA MPENZI WAKO AMEBADILIKA HUENDA UKAWA NA TABIA HIZI

Image
Kama unataka kulinda penzi lako lisiyumbe, hakikisha hauangukii kwenye mtego wa haya makosa ya kawaida yanayorudiawa sana. 1.Wivu Kupita Kiasi Wivu wa kipenzi ni wa kawaida, lakini ukizidi, unageuka kuwa mzigo. Anza kumuamini zaidi na kumpa uhuru. 2.Kupuuza Hisia Zake Mpenzi wako anahitaji kuungwa mkono kihisia. Kumpuuza kunaumiza kuliko unavyofikiria. 3. Kukosoa Kila Wakati Kosoa kwa kujenga, si kwa kumvunja. Kila mtu hupenda kuthaminiwa kwanza. 4. Kumuaibisha Hadharani Kumkejeli mbele za watu au mtandaoni humfanya ajisikie duni. Heshima ni muhimu kuliko "likes." 5.Kukosa Muda wa Pamoja Mapenzi yanakua kwa muda wa pamoja. Usipojitokeza, penzi linakauka taratibu. 6.Kutokuwa Mwaminifu Uaminifu ukivunjika, hata upendo mkubwa huanza kuyumba. Usaliti ni sumu ya penzi. 7.Kuzungumza Sana Bila Kumsikiliza Sikiliza kabla hujasema. Wakati mwingine, anachotaka ni tu sikio la kuelewa. 8. Kulinganisha na Wengine Kumlinganisha na ex wako au wengine humuumiza. Mpende kwa jinsi alivyo. 9.Ma...

EPUKA KULA NYAMA NYEKUNDU UNAPOONA DALILI HIZI

Image
Nyama nyekundu inaweza kuwa na virutubisho vingi na kuwa sehemu ya lishe bora, lakini si vyote miili yetu inaweza kuyadigest vyema. Watu wengi wanakutana na hali ya maumivu ya tumbo, maumivu ya kichwa, na uchovu baada ya kula nyama nyekundu. Ikiwa unakutana na dalili hizi, inaweza kuwa ishara kuwa mwili wako hauwezi kuchakata nyama vizuri. Hapa ni baadhi ya dalili muhimu za kuchunguza: Kupufuka Tumbo Ikiwa unapata kupufuka baada ya kula nyama nyekundu, inaweza kuwa ishara ya matatizo ya mmeng’enyo au kushindwa kuchakata chakula vizuri. Nyama yenye mafuta nyingi inaweza kuzalisha gesi mbaya inayosababisha kupufuka. Kutapika na Kuishiwa na Nguvu Dalili kama kutapika, kuungua tumboni, au kuhisi kichefuchefu baada ya kula nyama ni ishara nyingine ya kwamba mwili wako hauwezi kuchakata nyama vyema. Kupata Magonjwa Mara kwa Mara Ikiwa mwili wako hauwezi kuchakata nyama vizuri, unaweza kupata magonjwa mara kwa mara, hasa magonjwa ya kuambukiza kama salmonella au E. coli. Hii ni kwa s...

TUNDU LISSU AGOMEA KESI YA MTANDAONI

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga kutoa uamuzi kwa njia ya mtandao Aprili 28, 2025 kuhusu hoja za pingamizi za Mawakili wa utetezi katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu. Kesi hiyo imesikilizwa leo kwa njia ya mtandao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mhini ambapo upande wa Jamhuri kupitia Wakili wa Serikali Mwandamizi, Job Mrema umesema kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya Lissu kusomewa Maelezo ya Awali (Ph). Hata hivyo, upande wa Jamhuri kupitia Wakili Mrema ulipouliza mbona Mshtakiwa Lissu haonekani mtandaoni, Hakimu Mhini alimtaka Askari Magereza ajibu ambapo alisema kwamba Lissu amegoma kusomewa maelezo ya awali kwa njia ya mtandao (visual) ambapo Hakimu Mhini alirihusu kesi kuendelea pasipo Lissu kuonekana. Katika kesi hiyo Lissu anatetewa na Jopo la Mawakili 31 wakiongozwa na Wakili Mpale Mpoki ambaye aliungana na Alute Mugwai, Peter Kibatala na Jeremiah Ntobesya kuwasilisha mapingamizi, miongoni ...

TANZIA: WATU 7 WAFARIKI 15 WAJERUHIWA KATIKA AJALI

Image
Huzuni na simanzi vimetanda katika eneo la Luganga, lililopo katika Halmashauri ya Mji Mafinga, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa, baada ya kutokea kwa ajali mbaya iliyohusisha gari la kubeba wagonjwa (ambulance) na pikipiki ya matairi matatu aina ya Toyo. Katika mkasa huo uliojiri leo Jumamosi, Aprili 19, 2025, watu saba wamepoteza maisha kwa kushtukiza, huku wengine kumi na tano wakijeruhiwa vibaya baada ya ajali hiyo mbaya na kukimbizwa hospitali za Mufindi na Mafinga Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dk Linda Salekwa, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo yenye kuhuzunisha alipotembelea majeruhi waliolazwa. Akizungumza kwa masikitiko makubwa, Dk Salekwa alisema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa watu hao walikuwa safarini kuelekea mashambani kwa ajili ya shughuli zao za kila siku. Haikujulikana mara moja chanzo cha ajali hiyo, lakini ilielezwa kuwa gari la wagonjwa na toyo hiyo ziligongana, na kusababisha vifo na majeraha makubwa. "Ni ajali mbaya sana ambayo imetugusa sote. Tumepot...

TUNDU LISSU AHAMISHIWA UKONGA GHAFLA

Image
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa taarifa mpya kuhusu alipo Mwenyekiti wa Chama hicho Tundu Lissu baada ya jana kueleza kuwa walienda kumtembelea Keko na hawakumpata Chama hicho kimesema kuwa kinapenda kuuarifu umma kuwa mapema leo, tarehe 19 Aprili 2025, viongozi wakuu wa chama wamekutana na uongozi wa Jeshi la Magereza na kufahamishwa rasmi kuwa Mheshimiwa Tundu Lissu amehamishiwa katika Gereza la Ukonga. Kufuatia taarifa hiyo, familia, wanachama wa CHADEMA na watanzania wote waliokuwa na wasiwasi kuhusu mahali alipo Mheshimiwa Lissu, wanataarifiwa kuwa sasa wanaweza kumtembelea kwa kufuata taratibu za kawaida za kumuona mahabusu katika Gereza hilo. Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa Chadema Brenda Rupia amesema kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Bara, Mheshimiwa John Heche, anatarajiwa kufika Gereza la Ukonga leo kwa ajili ya kumwona Mheshimiwa Tundu Lissu na kuzungumza naye kuhusu hali yake. Jana Ijumaa Chadema walitoa taarifa kuwa viongozi wa Chama walifika Keko...

DALILI 10 ZINAZOONYESHA MKEO ANACHEPUKA NA HAKUPENDI

Image
Katika uhusiano wa kimapenzi, kuna nyakati ambapo unaweza kuhisi kuwa mambo hayako sawa. Hapa kuna dalili 10 ambazo zinaweza kuashiria kuwa mkeo ame cheat, pamoja na dalili 10 zinazoweza kuonyesha kuwa hakupendi tena. DALILI 10 ZINAZOASHIRIA MKEO AMECHEPUKA. 1.Mabadiliko ya Tabia Mkeo anaweza kuonyesha mabadiliko makubwa katika tabia yake. Anaweza kuwa na hasira, huzuni, au hata kuwa na furaha isiyo ya kawaida bila sababu. Hii inaweza kuwa ishara kwamba kuna mtu mwingine katika maisha yake. 2.Kujificha Simu Ikiwa mkeo anakuwa na siri kuhusu simu yake, kama kuificha au kuondoa ujumbe wa kawaida, hii inaweza kuwa dalili ya kuwa na uhusiano wa siri. Anapokuwa na wasiwasi kuhusu wewe kuona ujumbe wake, kuna uwezekano wa kuwa na kitu cha kuficha. 3.Muda wa Kuondoka Nyumbani Kama mkeo anaanza kutumia muda mwingi nje ya nyumba bila sababu za wazi, kama vile kusema anafanya kazi au anaenda kwa marafiki, hii inaweza kuwa dalili ya kuwa na uhusiano wa nje. 4.Kukosa Mawasiliano Kukosekana kwa maw...

LEMA AOMBA MUNGU SIMBA NA YANGA ZIFUTWE NCHINI

Image
Godbless Lema, mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ameendelea kukosoa mitazamo ya kisiasa ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam. Amesema kuwa wakazi hao hawajaonyesha msimamo wala mshikamano wa kudai mabadiliko ya kweli nchini. Lema alieleza kuwa hali hiyo ni changamoto kubwa katika harakati za kupigania haki na maendeleo ya taifa. Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara, Lema alisema kuwa wakazi wa Dar es Salaam wamekuwa nyuma katika jitihada za kudai haki. Alieleza kuwa badala ya kujikita katika masuala muhimu ya kitaifa, wakazi hao wamekuwa wakishabikia mambo yasiyo na tija. Alitaja michezo ya mpira wa miguu, hasa ushabiki wa timu za Simba na Yanga, kama moja ya mambo yanayowapotezea muda na nguvu Lema aliongeza kuwa hali hiyo inamkera sana, na anaamini kuwa taifa haliwezi kupata mabadiliko ya kweli bila watu kuwa na mwamko wa kisiasa. Alieleza kuwa kushabikia soka kupita kiasi kunawafanya wananchi wasione umuhimu wa kushiriki katika masuala muhimu ya tai...

JINSI MWANAMKE ANAVYONYESHA HISIA ZAKE

Image
Mwanamke anaweza kukuonyesha hisia zake kwa njia mbalimbali, ambazo zinaweza kuwa za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja. Hapa kuna baadhi ya njia ambazo mwanamke anaweza kuonyesha hisia zake: 1.Mawasiliano ya Kinywa Mwanamke anaweza kuonyesha hisia zake kupitia maneno anayoyatumia. Maneno ya upendo, sifa, au hata maswali yanayoonyesha kujali yanaweza kuwa ishara kwamba anavutiwa nawe. Kwa mfano, mwanamke anapokutaja mara kwa mara au kuonyesha hamu ya kujua zaidi kuhusu wewe, hii inaweza kuwa ishara ya hisia za kimapenzi. 2.Mawasiliano ya Mwili Mwanamke anaweza pia kuonyesha hisia zake kupitia lugha ya mwili. Hii inaweza kujumuisha: Kuangalia macho: Ikiwa anakuangalia kwa muda mrefu, hii inaweza kuwa ishara ya kuvutiwa. 3.Kugusa : Kugusa kidogo mkono wako au bega lako wakati wa mazungumzo kunaweza kuashiria hisia za karibu. 4.Miondoko ya mwili: Kujiweka karibu nawe au kuonyesha mabadiliko ya mkao wakati wa mazungumzo kunaweza kuonyesha kuwa anajisikia vizuri katika uwepo wako. 5....

CHAMA IKATAA YANGA MOJA KWA MOJA

Image
Mchezaji mahiri wa Young Africans, Clatous Chama, ameibua gumzo lingine kwenye mitandao ya kijamii. Inaripotiwa kuwa kiungo huyo fundi amefuta (unfollow) akaunti rasmi ya klabu yake ya Young Africans kwenye mtandao wa Instagram. Jambo la kushangaza zaidi ni kwamba, Chama ameanza tena kuifuatilia (follow) akaunti ya klabu yake ya zamani, Simba SC, ambayo aliifuta alipojiunga na Yanga. Kitendo hiki kimeacha maswali mengi kwa mashabiki wa soka nchini Tanzania. Je, hii ina maana gani? Kuna nini kinachoendelea nyuma ya pazia? Wengi wanasubiri kwa hamu kujua hatima ya kiungo huyo mwenye uwezo wa kubadilisha mchezo. Hii si mara ya kwanza kwa Chama kufanya vitendo vinavyozua uvumi kuhusu uhamisho wake. Mashabiki wanasubiri kwa shauku kujua kama huu ni mwanzo wa kurejea kwake Simba SC au ni mchezo mwingine wa akili kwenye ulimwengu wa soka. Kwa upande wa baadhi ya mashabiki walidai kuwa, Kiungo huyo kutoka Zambia tayari yupo katika harakati za kuagana na wanajangwani kutokana na kukosa nafasi k...

CHADEMA YAFUNGIWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OCTOBER 2025

Image
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Huru ya Taifa ya Uchaguzi – INEC Ramadhani Kailima amesema Chama cha Demokrasia na maendeleo - CHADEMA hakitoshiriki Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2025 na chaguzi zote ndogo kwa muda wa miaka mitano kufuatia kutosaini kanuni za maadili ya Uchaguzi. Kailima amsema hayo mara baada ya zoezi la kusini kanuni za maadili ya Uchaguzi leo April 12, 2025 katika ofisi za Tume hiyo Njedengwa Jijini Dodoma ambapo vyama vya siasa 18 ndivyo vimesaini isipokuwa CHADEMA. “Chama cha CHADEMA ambacho hakikusaini kanuni za maadili ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani wa mwaka 2025, hakitashiriki uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu na chaguzi zote ndogo zitakazofuata kwa muda wa miaka mitano.” Ramadhan Kailima mkurugenzi wa Tume huru ya Uchaguzi. Mapema asubuhi hii, Katibu mkuu wa chama hicho alinukuliwa katika mitandao ya kijamii alisema: "Katibu Mkuu CHADEMA sitakuwepo kwenye kikao cha tarehe 12 Aprili 2025 cha kushauriana na kusaini ...

MWANDISHI NYANDA HATIANI KUMLIPA DED UBUNGO BILIONI 2

Image
Mwandishi wa habari kutoka Kampuni ya Sahara Media Group na mwendeshaji wa kipindi cha The Big Agenda Aloyce Nyanda ametiwa hatiani kwa kosa la kumdhalilisha mitandaoni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Ubungo Aron Kagurumjuli. Baada ya kutiwa hatiani Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza, Nyanda amemhukumu kumlipa fidia ya Sh.billioni mbili Mkurugenzi aliyedhalilisha katika moja ya machapisho yake mtandaoni. Akisoma hukumu hiyo ya kesi ya madai ya udhalilishaji namba 6166/2024 leo Aprili 11, 2024, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Bonaventure Lema amesema baada ya kusikiliza mpande mbili Nyanda alikutwa na hatia ya kumdhalilisha Mkurugenzi huyo kupitia mitandao yake ya kijamii. Amesema kosa hilo ni kinyume cha Sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari ya mwaka 2016 kifungu cha 35. Imeandikwa na Mwandishi Wetu,Mwanza CHANZO CHA HABARI  NIPASHE.

FANYA HAYA KWA MPENZI WAKO NAYE ATAKUPENDA SANA

Image
Kuna mambo ya msingi ambayo wanawake huyathamini sana kutoka kwa wapenzi wao wa kiume, ingawa mara nyingi huwa hawayasemi waziwazi. Lakini ukiyazingatia na kuyatekeleza, ni vigumu mwanamke aliyewahi kuwa na wewe kukusahau, hata kama uhusiano wenu utakoma 1. Kuheshimiwa : Heshima ni nguzo muhimu kwa mwanamke katika mahusiano. Wanawake hawapendi kuitwa kwa majina ya kudhalilisha kama vile “mjinga” au “malaya”, na hawapendezwi kabisa na kulinganishwa na wanawake wengine kwa njia ya kuwashusha hadhi. Pia, ukimkosea heshima mbele za watu, hata kwa jambo dogo, huweza kuharibu sana hisia zake kwako. 2. Kuwekwa Mbele na Kupewa Kipaumbele : Wanawake hupenda kujua kuwa wao ni wa muhimu kuliko mtu yeyote katika maisha ya mwenzi wao. Kumpenda si tu kumweka kwenye ndoa au uchumba, bali ni kumthamini kila siku. Mwanamke anapenda kuwa wa kwanza kwa mwenzi wake katika mazungumzo, mipango, na maamuzi ya kila siku bila kuhisi kama kuna mwingine anayemzidi kwa nafasi. 3 . Uhuru wa Kujieleza:   Ni muhimu...

LISSU ALEGEZA MASHART YA CHADEMA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU

Image
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA, Tundu Lissu amelegeza masharti kuhusu chama hicho, kushiriki uchaguzi akitaka mambo sita yafanyikie ili waingie katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Lissu ametaja mambo hayo ni kubadilishwa kwa mfumo wa uchaguzi ili kusiwe na mgombea anayepita bila kupingwa, watoto wadogo wasiandikishwe kwenye daftari la kudumu la mpigakura, kukomeshwa engua engua ya wagombea wa upinzani. Kwa mujibu wa Lissu, mengine ni wagombea wa upinzani wasifanyiwe vurugu kwenye kampeni, mawakala hasa wa vyama vyote wafanye shughuli zao bila usumbufu na uchaguzi usiwe sehemu ya kutoa kafara ili kupata viongozi. Lissu alieleza hayo Aprili 8, 2025 wakati akizungumza na wananchi wa Namtumbo mkoani Ruvuma, akitokea wilaya za Masasi na Nanyumbu mkoani Mtwara katika mwendelezo wa ziara ya chama hicho, kunadi ‘No Reforms No Election. Masharti haya aliyotoa Mwenyekiti Lissu hayajajumuishi mambo ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele hapo awali hususan ma...

MUSEVEN AWAPA WABUNGE SHILINGI MILIONI 100 KILA MMOJA

Image
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ameripotiwa kuwapa baadhi ya wabunge zawadi ya Shilingi milioni 100 kila mmoja, ikiwa ni sehemu ya kile kinachoelezwa kuwa ni “shukrani kwa tabia njema.” Wabunge waliopokea fedha hizo wanatoka katika chama tawala cha National Resistance Movement (NRM), pamoja na wabunge wa vyama vya upinzani na wale wa kujitegemea (independent). Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu na tukio hilo, wabunge wa NRM walichukua fedha hizo kati ya saa mbili usiku na saa tatu usiku mnamo Aprili 7, kutoka ofisi ya Government Chief Whip bungeni. Wengine wameripotiwa kupokea pesa hizo moja kwa moja kutoka kwa Spika wa Bunge, Anita Among, katika makazi yake ya Nakasero. Taarifa zinadai kuwa zawadi hiyo imetolewa kufuatia maombi ya wabunge waliokuwa wakikabiliwa na hali ngumu ya kifedha, na ni kama ishara ya kutambua ushirikiano wao na serikali. Hata hivyo, taarifa hizo zimeibua maswali mengi kuhusu uwazi na matumizi ya rasilimali za umma. Msemaji Msaidizi wa Ikulu, Faruk Kirunda, alipoh...

WABUNGE TANGA TUMBO JOTO

Image
TANGA – Hali si shwari miongoni mwa baadhi ya wabunge wa Mkoa wa Tanga huku ripoti zikionesha kuwapo kwa sintofahamu, wasiwasi na presha ya kisiasa inayowakumba baadhi yao. Chanzo kikuu cha hali hiyo ni mabadiliko ya kisiasa yanayotarajiwa kuelekea uchaguzi mkuu ujao pamoja na presha kutoka kwa wapiga kura na chama chao. Taarifa zinaeleza kuwa baadhi ya wabunge wameanza kuhisi mdororo wa uungwaji mkono kutoka kwa wananchi kutokana na madai ya kutotimiza ahadi walizozitoa kipindi cha kampeni. Wengine wanadaiwa kuwa na mvutano na viongozi wa chama ngazi ya mkoa na wilaya, jambo linalotishia nafasi zao katika mchakato wa kura za maoni. Sababu Zinazowafanya Wabunge Hao Kuweweseka: 1 . Kasi ya Wapinzani wa Ndani ya Chama:  Kumekuwa na taarifa kuwa baadhi ya makada wa chama tawala wameanza kampeni za chinichini kutafuta nafasi za kugombea ubunge, wakilenga majimbo yanayoshikiliwa na wabunge waliopo sasa. Hali hii imewaweka wabunge kwenye wakati mgumu wakihofia kupoteza tiketi ya chama. 2. Ma...

WAZIRI MKUU KUWASILISHA BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU NA BUNGE KESHO

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, anatarajiwa kuwasilisha hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Bunge kwa mwaka wa fedha 2025/2026 leo, Jumatano Aprili 9, kuanzia saa 4:00 asubuhi katika ukumbi wa Bunge jijini Dodoma. Hotuba hiyo itakuwa ni sehemu muhimu ya mchakato wa kupanga na kuelekeza matumizi ya serikali kwa mwaka ujao wa fedha, ambapo wananchi, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo wanatazamia kusikia vipaumbele vya serikali, mafanikio yaliyofikiwa katika mwaka uliopita, pamoja na mikakati mipya ya kukuza uchumi na kuboresha huduma kwa wananchi. Taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu zinaeleza kuwa hotuba hiyo itatangazwa moja kwa moja (mubashara) kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo televisheni, redio na mitandao ya kijamii, ili kuwawezesha Watanzania wote kufuatilia kwa karibu mijadala na maamuzi muhimu yatakayowekwa mezani. Miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kupewa kipaumbele katika bajeti hiyo ni ajira kwa vijana, ub...

ELON MUSK AMVAA TRUMP HADHARANI, AKOSOA HAYA MAAMUZI YAKE

Image
Elon Musk, bilionea maarufu na mshauri wa Rais Donald Trump, amekosoa hadharani sera ya ushuru ya Rais Trump, na kutoa wito wa kuanzishwa kwa biashara huria na mazingira ya ushuru sifuri. Musk, ambaye ni miongoni mwa watu matajiri zaidi duniani, aliweka wazi mtazamo wake kuhusu mpango wa Rais Trump wa kuweka ushuru mkubwa kwa bidhaa za kuagiza kutoka nje, hususan kutoka China. Hii ni baada ya Trump kutangaza kuwa atafanya mageuzi ya ushuru kwa bidhaa nyingi za kimataifa, na kuongeza ushuru wa 50% kwa bidhaa kutoka China, kwa kuongeza ya ushuru wa awali wa 34%. Musk, ambaye amekuwa mshauri wa Trump na amekuza urafiki wake na Rais huyo kupitia uwekezaji wake wa karibu $290 milioni kwenye kampeni ya Trump, alieleza kuwa hakubaliani na sera hii ya uchumi inayohusisha ushuru mkubwa. Katika mtandao wa kijamii, Musk alieleza wasiwasi wake kuhusu sera hii na kumshauri Rais Trump kupitia ujumbe wa moja kwa moja ili kupunguza athari za masharti ya biashara makali. Alimkosoa moja kwa moja mshauri...

MAMA FEI TOTO AITIKISA YANGA, AMPELEKA MWANAE SIMBA

Image
Nyota wa Klabu ya Azam, Feisal Salum 'Fei Toto' huenda akajiunga na klabu ya Simba mwishoni mwa msimu huu licha ya kutakiwa na klabu ya Yanga ambayo aliwahi kuitumikia kwa mafanikio makubwa kwa misimu kadhaa. Taarifa hii imekuja mara baada ya Mchambuzi wa michezo kutoka E FM, Wilson Oruma, Aprili 8, kuweka wazi kuwa vita bado ni mbichi kwa vilabu vya Simba na Yanga kwenye harakati za kuhakikisha wanainasa saini ya Feisal Salum. Katika sakata hilo, klabu ya Yanga imeonesha nia kubwa ya kutaka kunasa saini ya nyota huyo, lakini klabu ya Simba nayo imeonesha nia kubwa ya kumtaka nyota huyo kikosini ikiwa ni njia moja wapo ya kuboresha kikosi. Licha ya Yanga kuonekana kuwa wapo tayari kutoa hadi nyumba, dili lake na Fei Toto limeonekana kuwa gumu baada ya mama mzazi wa mchezaji huyo kuingilia kati dili hilo. Ambapo imeripotiwa kuwa hataki arudi tena Yanga Kufuatia kile alichopitia klabuni hapo. Ikumbukwe kuwa, kipindi Feisal Salum anaondoka Yanga kwenda Azam FC kulitokea na sintofa...

MWANAUME ACHA HIZI "K" TATU KUEPUKA UMASIKINI

Image
Mwanaume ni mtu ambaye ameumbwa na mwenyezi mungu kwajili ya kuongoza dunia na vitu vyake vyote akiwema mwanamke ndani yake. Siku ya leo nakuletea "K" hizi tatu ambazo mwanaume akiziendekeza basi anaweza kuwa masikini wa kutupwa yeye na familia zake, lakini endapo akiziogopa basi anaweza kusahahu swala la umasikini kwenye maisha yake. "K" ya kwanza ni kula sana. Mwanaume unapokua katika upo katika hali ya kujitafuta hutakiwi kuweka chakula kama kitu cha msingi sana. Hapa namaanisha mfano mwanaume umepata shilingi elfu 10 hakikisha unatumia kiasi kidogo kwenye chakula kuliko kinachobaki. Wataalamu wanasema kwamba endapo mwanaume utaweza kuondokana na dhana hii ya kula sana alafu ela yako kubwa ukawekeza kwenye mambo mengine, basi kuna asilimia kubwa sana ya wewe mwanaume kufanikiwa kwenye maisha yako. Lakini ukitaka kuwa masikini wa kutupwa basi endekeza kula. Leo umepata elfu 20 unataka ukale chakula cha elfu 15 ubaki na robo ya ela hiyo. Lakini pia kumbuka hata mke...

TUNDU LISSU ASHAMBULIWA NA WANANCHI BAADA YA KUTANGAZA MAANDAMANO NCHI NZIMA

Image
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema ndugu Tundu Lissu amekiona Cha Moto Baada ya Kutangaza maandamano siku ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi wa 10 mwaka huu, na hiyo ni kama Serikali kupitia Tume huru Ya Uchaguzi itachishidwa Kuweka utaratibu sawa kuelekea uchaguzi huo. Wananchi ambao wametoa maoni Yao wameonesha kuchukizwa na kauli ya Tundu Lissu ya Kutaka wananchi kuandamana Nchi nzima wakati uchuguzi ukiendelea, wengi wao wakiamini kufanya hivyo ni kuhatarisha usalama wa Raia na Mali zao. Itakumbukwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu aliweka bayana na kusema kuwa siku ya uchaguzi mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu, chama hicho kitaitisha maandamano ya kuuzuia uchaguzi usifanyike. Kauli hiyo ya Lissu, inajibu swali kuhusu mbinu ambayo chama hicho itaitumia kuzuia uchaguzi kuendana na ajenda yake ya ‘No Reforms, No Election’ (bila mabadiliko, hakuna uchaguzi). Kauli ambao kwa wanachadema wanaona ni rafiki na n...

FAHAMU SEHEMU ZA MWILI ZISIZOHISI MAUMIVU

Image
 Ukweli Unaoshangaza Kutoka WHO. Unapofikiria kuhusu maumivu, mara nyingi akili yako huenda moja kwa moja kwenye ajali, kuungua au hata meno yanapouma. Lakini je, umewahi kujiuliza kama kuna sehemu za mwili ambazo hazihisi maumivu kabisa? Swali hili linaweza kuonekana la ajabu, lakini jibu lake linashangaza zaidi! Shirika la Afya Duniani (WHO) na wataalamu wa afya duniani kote wamekuwa wakifanyia kazi uelewa wa mfumo wa maumivu mwilini, na baadhi ya matokeo yake ni ya kushangaza kabisa. Katika makala hii, tutaangazia sehemu tano kuu za mwili ambazo hazihisi maumivu, kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kitabibu, vikiwemo vyanzo vya WHO. Pia, tutagusia kwa nini sehemu hizi hazihisi maumivu na umuhimu wake katika matibabu. 1. Nywele – Uzuri Usiohisi Maumivu Nywele ni moja ya sehemu za mwili ambazo hazina mishipa ya fahamu. Hii ina maana kuwa huwezi kuhisi maumivu unaponyoa au kukata nywele zako. Hii ndiyo sababu unaweza kunyolewa bila ganzi wala dawa yoyote ya kupunguza maumivu. Kwa nini n...

MICHEZO: RASMI SASA FEI TOTO KURUDI YANGA, AZIKOSA OFA HIZI

Image
Katika hatua mpya ya kusisimua kwenye dirisha la usajili, klabu ya Yanga SC imeingia rasmi kwenye mazungumzo na kiungo wa Azam FC, Feisal Salum maarufu kama Fei Toto, kwa lengo la kumsajili tena na kumrejesha Jangwani. Jioni ya jana, viongozi wa Yanga wamekutana na wawakilishi wa mchezaji huyo kuwasilisha pendekezo lao rasmi. Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, ofa iliyotolewa na Yanga (hasa katika malipo ya awali ya usajili - sign-on fee) ni kubwa zaidi kuliko ile ya wapinzani wao wa jadi, Simba SC. Ikumbukwe kuwa Yanga inatarajia kumuuza nyota wao Aziz Ki mwishoni mwa msimu huu, huku mchezaji mwingine wa nafasi hiyo, Pacome, akiwa bado hajasaini mkataba mpya. Hii inawasukuma viongozi wa Yanga kumtazama Fei Toto kama chaguo mbadala lenye ubora. Kwa sasa, Fei Toto anashikilia jumla ya ofa tatu kutoka ndani ya Tanzania: 1. Ofa ya mkataba mpya kutoka Azam FC. 2. Ofa ya usajili kutoka Simba SC. 3. Ofa kubwa (mega deal) kutoka Yanga SC. Hata hivyo, kikwazo kikuu kinachoweza kuzuia ku...

MAISHA: MAMBO YA KUZINGATIA KWENYE PENZI JIPYA

Image
Karibu kwenye safari mpya ya mapenzi! Kuanzisha uhusiano mpya ni kama kupanda maua—yanahitaji uangalizi, subira, na msingi imara ili yastawi.Hapa nakuletea mambo matano muhimu ya kuzingatia ili uweze kujenga penzi linalofana na kukuza furaha yako. 1. Jijue Mwenyewe Kwanza Kabla ya kuingia kwenye penzi, chunguza moyo wako. Unataka nini kweli kwenye uhusiano? Maadili yako ya msingi ni yapi? Kujua unachotamani na unachokataa kutavumilia kutakusaidia kuweka mipaka yenye afya na kuepuka mkanganyiko baadaye. Penzi linalofanikiwa huanza na uelewa wa ndani kabisa wa nafsi yako. 2. Mawasiliano ya Wazi ni Gundi Tangu mwanzo, jenga tabia ya kuongea wazi na kwa uaminifu. Shiriki hisia zako, matarajio yako, na hata woga wako. Usifikirie kwamba mpenzi wako atasoma akili yako—sema unachofikiria kwa upole na heshima. Mawasiliano mazuri ni kama maji kwa mmea; yanadumisha uhai wa penzi. 3. Uvulimivu Usikimbilie kila kitu mara moja. Penzi jipya ni kama divai nzuri—inahitaji muda ili ladha yake iwe kamil...

YANGA VS COASTAL UNION LEO

Image
MATOKEO Yanga Vs Coastal Union Leo Tarehe 07 April 2025 Young Africans itamenyana na Coastal Union katika mechi ya Ligi Kuu Bara ya Tanzainia Aprili 7. Mechi hiyo inatarajiwa kuanza saa 16:00 kwa saa za kwenu. Miezi 5 baada ya mechi zao za mwisho za Ligi Kuu Bara, Young Africans na Coastal Union zinatarajiwa kumenyana tena. Katika mechi yao ya mwisho, Young Africans walipata ushindi wa 0-1. Kwa ushindi wa timu za Tabora United, Songea United, Pamba Jiji, Mashujaa, Singida Black Stars na MC wa Kinondoni, Young Africans inazidi kusonga mbele na kufikisha michezo kumi na saba ya kutopoteza. Hivi majuzi, juhudi zao za ulinzi zimekuwa thabiti, na kuweka safu nne safi mfululizo. Coastal Union, kwa kulinganisha, inaelekea kwenye mchezo huu kufuatia kipigo kutoka kwa Kagera Sugar kwenye Ligi Kuu Bara Alhamisi iliyopita, ikiwa ni mechi saba bila ushindi hata mmoja.