AZAM FC YAMTIMUA KOCHA OMOG

OMOG

Kipigo cha mabao 3-0 ugenini dhidi ya El-Merrikh ya Sudan, kimemponza kocha Joseph Omog baada ya uongozi wa Azam FC kuamua kumtimua.
Kwa mujibu wa taarifa iliyowekwa kwenye mtandao wa facebook wa Azam FC muda mfupi uliopita, Uongozi wa Azam FC umetangaza kumtimua raia huyo wa Cameroon.
Taarifa hiyo inasomeka: “Uongozi wa Azam FC unatangaza kuachana na kocha wake mkuu Joseph Omog baada ya kuwa naye kwa miezi 14.
Omog aliyeipa Azam FC ubingwa wa kwanza msimu uliopita ameondoka pamoja na msaidiI wake Ibrahim Shikanda.
Kwa sasa timu itakuwa chini ya George Best Nsimbe.”

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA