SOFIA SIMBA: RAIS KIKWETE HAJASAINI MSWADA WA SHERIA YA MTANDAO, LAKINA SIO MREFUI ATAUSAINI MUD



Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Sophia Simba (kulia), akikata utepe kuzindua rasmi Taasisi ya maendeleo ya jamii ya Sitti Tanzania Foundation iliyofanyika Dar es Salaam juzi (kushoto) ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Sitti Mtemvu.

Na Mwandishi Wetu, Mpekuzi-Dar es Salaam
WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, amesema kuwa kutokana na hali ya nchi kwa sasa Rais Jakaya Kikwete, atasaini sheria ya mtandao.
 
Kauli hiyo aliitoa jana  baada ya kuripotiwa na gazeti moja la kila siku mwishoni mwa wiki katika uzinduzi wa Kitabu cha Chozi la Sitti, ambapo alinukuliwa akisema kuwa Rais Kikwete ameshasaini sheria hiyo.
 
Akikanusha taarifa hiyo alisema kuna uwezekano amenukuliwa vibaya ila usahihi wa kile alichosema ni kwamba Rais ataisaini sheria hiyo kutokana na hali ya usalama wa nchi kwa sasa.
 
Nilishosema si kwamba sheria imesainiwa, maana kwa mujibu wa utaratibu wa sheria ni kwamba sheria yoyote rais akishaisaini inapelekwa taarifa kwa Spika wa Bunge ambaye naye huitangaza.
 
“Kwa hiyo nami katika uzinduzi ule nilisema kama kukazia kauli ya Ikulu kuwa Rais Kikwete ataisani sheria ile kwani imefuata taratibu zote, ikiwemo kujadiliwa bungeni na hatimaye kuridhiwa.
 
“Hivyo ninawaomba Watanzania, waelewe kuwa hiki ndicho nilichokisema na si vinginevyo,” alisema Sophia.
 
Waziri huyo alisema pamoja na mitandao ya kijamii kusaidia kuleta maendeleo na kusambaza taarifa kwa muda mfupi, lakini kuna watu wamekuwa wakiitumia vibaya ikiwemo kuchafuana huku anayeathirika akishindwa kuchukua hatua za kisheria.
 
Pamoja hatua hiyo wadau wengi wamekuwa wakimshauri Rais Jakaya Kikwete asiisaini sheria ili kwani inaminya na hata kunyonga uhuru wa habari nchini.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA