TCRA WAMEFANIKIWA KUZIMA SIMU LAKI SITA (600,000) ZOEZI LINAENDELEA



Uzimaji wa Imei bandia ulifanyika usiku wa kuamkia jana kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) katika simu zaidi ya 600,000 zenye Imei batili. 

Kwa mujibu wa TCRA, Imei ni namba ya kimataifa ya utambuzi wa vifaa vya kielektroniki, ikiwamo simu. Ina tarakimu 15 ambazo ni za kipekee kwa kifaa husika na zinatambulika kimataifa. Namba hizo hutumika kudhibiti bidhaa bandia au simu kutumiwa na mtu mwingine. 

Jana, Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy alisema takwimu hizo ni zile ambazo zimetokana na kazi ya kukata mawasiliano katika simu bandia iliyofanyika kuanzia saa sita usiku mpaka saa kumi alfajiri ya jana. 

Alisisitiza kuwa mtambo huo unaendelea na kazi kuhakikisha kuwa hata simu ambazo hazipo au hazikuwa hewani zitakapowashwa hazitafanya kazi. 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

JINSI YA KUKAA NA NGUVU ZA MUNGU SEHEMU YA KWANZA