Posts

N'GWANA MALUNDI MTU WA UMBILE LA AJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KWENYE JAMII YA WASUKUMA

HEBU LEO MJUE VIZURI HUYU MTU WA MIUJIZA AITWAE NG'WANAMALUNDI SHUJAA WA WAKISUKUMA ALIYEWATESA WAJERUMANI. Kwa wale waliopata kusoma historia au kusikia hadithi za makabila, hasa ya Wasukuma na Wanyamwezi, hawakukosa kusikia habari ya Ng’wanamalundi. Mtu huyo aliyewahi kuutingisha utawala wa Wajerumani, alizaliwa katika ukoo wa kawaida akiwa mcheza ngoma mashuhuri, mwaka wa kuzaliwa kwake haufahamiki ila alifariki dunia mwaka 1936, akiwa tayari mtu mzima. Watu wengi wamekuwa wakimjadili kwa maoni tofauti, wengine wakimsifu kama shujaa huku wengine wakihusisha uwezo wake na nguvu za giza. Katika makala hii usahihi wa historia yake unaelezwa na mjukuu wake wa pili, Kishosha Sitta (80) mkazi wa Kijiji cha Mwalugulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, anayesimulia alivyomfahamu babu yake huyo. Sitta anaanza kueleza kuwa jina halisi la babu yake halikuwa Ng’wanamalundi bali lilikuwa Igulu Bugomola, ambaye alizaliwa katika Kijiji cha Mwakubunga Nera wilayani Kwimba mkoani Mwanza....

ALIKIBA NA BARNABA WALIVYOWASILI CLOUDS NA BIBI HARUSI WAO

Image

Sababu za Roberto Carlos kuamini CR7 ni bora kuliko Messi

Image
Mjadala mkubwa katika soka ulimwenguni kwa sasa ni juu ya uwezo wa wachezaji wawili mmoja anakipiga Real Madrid na mwingine yuko Barcelona pale, ndio ni Cristiano Ronaldo na Lioneil Messi. Mjadala wa Messi na Ronaldo unaonekana mpana sana na kila mtu ana sababu zake kumkubali huyu na kumkataa huyu, na hata kwa beki wa zamani wa Brazil Roberto Carlos naye ana sababu za kumkubali zaidi CR7. Carlos anaamini kwamba Cristiano Ronaldo ni bora zaidi ya Lioneil Messi kwani amekuwa akimuona Ronaldo mazoezini jinsi amekuwa akijituma na pia juhudi zake mazoezini anavyozionesha uwanjani. Carlos anasema tofauti kati ya Messi na Ronaldo ni kwamba Ronaldo anajituma sana akiwa uwanjani na pia mazoezini kiyu ambacho Lioneil anaonekana kukikosa na zaidi anaamini katika kipaji chake. Carlos amewahi kuichezea Real Madrid kwa miaka zaidi ya 14 kabla yakuondoka kutoka kwa wababe hao wa Hispania mwaka 2007 ambapo alikwenda kujiunga na klabu ya Fernabache ya nchini Uturuki.

HABARI ZILIZOPO KWENYE MAGAZETI YA LEO JAN 5. 2018

Image
Friday, January 5, 2018

UAMUZI WA KAMATI YA UTENDAJI TFF KUHUSU ATAKAYEKAIMU NAFASI YA MALINZI KWA SASA

Image
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, iliyokutana jana  Jumamosi Julai 01, 2017 kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam imempitisha Wallace Karia kuwa Kaimu Rais wa shirikisho. Kadhalika, Kamati hiyo ya Utendaji ya TFF, imempitisha Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF. Viongozi hao watakaimu nafasi hizo tajwa hadi hapo mahakama itakavyoamua kuhusu kesi zinazowakabili kwa sasa Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Katibu Mkuu, Mwesigwa Selestine.  Kamati ya Utendaji ya TFF, imekutana kwa dharura kwa mujibu wa Ibara ya 35 (1) inayosomwa pamoja na Ibara ya 35 (6) na kufanya uamuzi huo. WAPITISHWA KUWANIA NAFASI MBALIMBALI TWFA Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu kwa Wanawake (TWFA), imetangaza majina ya wagombea 11 waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika Julai 8, mwaka huu mkoani Morogoro. Majina ambayo yamepitishwa ni Amina Karuma, Rose Kisiwa,...

MAJINA YA WAUAJI KIBITI HAYA HAPA , WAANZA KUSAKWA NCHI NZIMA

Image
                          

KAULI ZA MAWAKILI BAADA YA MALINZI NA MWESIGWA KUNYIMWA DHAMANA

Image
Baada ya mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kuwanyima dhamana Rais wa TFF Jamal Malinzi, Katibu Mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa na afisa wa fedha Nsiande Mwanga, jopo la mawakili wa utetezi wameonekana kutoridhika na wateja wao kukosa dhamana. “Washtakiwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani halafu wanaomba tena upelelezi wa kesi wakati suala tayari lipo mahakamani hiyo ndio pointi kubwa ambayo tumeiibua halafu kitu kingine tulichokiibua ni pamoja na maombi ya dhamana,”  Jarome Msemwa-wakili upande wa utetezi. “Tumeiomba mahaka itoe dhamana kwa wateja wetu, kuna sheria ya Bunge inayokataza dhamana halafu kuna katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoruhusu dhamana. Kwa hiyo kwa amri ya mahakama ambayo imesomwa leo (jana) wateja wetu wanapelekwa rumande hadi Jumatatu Julai 3, 2017.” “Sikutarajia katika muda na wakati kama huu kutakuwa na mashitaka yanayowakabili yanayofika 28 ya aina ileile lakini ndani yake yanatengenezwa machache kufanywa ya tutakatisha fedha wakati mash...