Posts

WALAJI WA MBOGA ZA MAJANI JIJINI DAR KIFO KINAWANYEMELEA

Image
Mkulima akichuma mchicha katika shamba lake maeneo ya Keko Mwanga jijini Dar es Salaam.  -Hulimwa mabonde ya Msimbazi,Ubungo.   -Hatarini kuugua,figo saratani ini na ubongo.  Wakazi WA jiji la Dar es Salaam wako katika hatari ya kupatwa na magonjwa makubwa kama saratani, utasa, kupoteza uwezo wa kuona, kuharibu ubongo, maini na figo, kutokana na matumizi ya mboga za majani zinazolimwa katika mabonde ya jiji hilo, NIPASHE imebani Matumizi ya mboga hizo ni makubwa jijini humo, yakitokana na umuhimu wake kwa afya za watu na hali duni ya maisha inayozifanya familia nyingi kumudu gharama zake ikilinganishwa na vitoweo vingine. Sehemu kubwa ya mboga hizo inatokana na kilimo kinachofanyika kwenye bonde la Mto Msimbazi na maeneo ya Kigogo-Sambusa, Ubungo--Gereji, Mchicha – Vingunguti na Tandale. Tayari matokeo ya tafiti kadhaa yamedhihirisha maji yanayotumika kwa umwagiliaji wa mboga za majani jijini humo kuwa na kemikali zenye sumu ama taka zinazotoka viwandani na kwenye ma...

MFANYAKAZI WA SALUNI AFIA GESTI

Image
Mwili wa Ramadhan ukipakizwa kwenye gari la polisi. Kifo hakina huruma! Msusi wa saluni ya wanawake iitwayo HK iliyopo mjini hapa, aliyetambuliwa kwa jina moja la Ramadhan almaarufu Rama anadaiwa kufia katika nyumba ya kulala wageni (gesti) na kuibua utata mkubwa, kwani alikwenda kulala akiwa fiti kabisa hivyo polisi kupewa kazi ya kuchunguza kubaini kilichomuua. Kwa mujibu wa mashuhuda wetu, tukio hilo lilijiri wiki iliyopita kwenye Gesti ya Salama iliyopo Gongoni Manispaa ya Tabora mjini hapa ambapo lilikusanya umati kwa kuwa Rama alikuwa akifahamika kwa wengi. Ilifahamika kwamba Rama aligundulika ‘amededi’ baada ya kutoamka hadi mchana. Anayedaiwa kuwa mpenzi wake Ramadhan akiwa kwenye gari la polisi. Ilisemekana kwamba baada ya kuona mazingira hayo ya kutatanisha, mhudumu aliita polisi ambao walifika na kuvunja mlango ndipo wakamkuta jamaa akiwa marehemu. Kwa mujibu wa mhudumu huyo, ilikuwa ni siku ya tatu mfululizo kwa Rama kulala mahali hapo ambapo usiku wa tukio a...

MAGAZETI YA LEO DESEMBA 10

Image
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

IKULU HAITAWAADHIBU VIGOGO WA ESCROW BILA YA UCHAGUZI.

Image
Ikulu imesema pamoja na kuwa Rais Jakaya Kikwete amekwishapokea maazimio ya Bunge kuhusu wanaotuhumiwa kuchota Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow, hawezi kuwachukulia hatua mpaka hapo uchunguzi kuhusu suala hilo utakapokamilika. “Rais lazima aagize vyombo vya uchunguzi kufanya kazi yake na baada ya hapo ndipo atapata mahali pa kuanzia. Watu wengi walitaka Rais Kikwete achukue hatua baada ya kupewa maazimio ya Bunge. Jambo hilo haliwezekani,” Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema jana na kuongeza kuwa hatua zitachukuliwa kwa watakaobainika kuwa na makosa ya kimaadili au jinai baada ya uchunguzi. Alisema uchunguzi kuhusu uchotwaji wa mabilioni hayo uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) pia utazingatiwa na Rais katika kutoa uamuzi. “Maazimio ya Bunge ni mazuri ila inatakiwa muda kwanza ili Rais naye apate taarifa za uchunguzi zaidi. Maazimio hayo ni muhimu na s...

DAVIDO AKERWA NA USHINDI WA IDRIS

Image
Msanii wa Muziki wa Kinigeria maarufu kama Davido iliyo onyesha wazi kukerwa na ushindi wa Idris wa Tanzania katika Shindano la Big Brother huko Afrika Kusini Davido amedai udanganyifu umefanyika. 

MAGAZETI YA LEO DESEMBA 8

Image
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .. . . . .